Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waasi wa CNDP wakumbushwa na UNHCR kuhishimu haki halali za wahamaji waliopo Rutshuru katika JKK

Waasi wa CNDP wakumbushwa na UNHCR kuhishimu haki halali za wahamaji waliopo Rutshuru katika JKK

Shirika la UNHCR limetoa mwito maalumu unaowataka waasi wafuasi wa kundi la CNDP la Laurent Nkunda, katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) kuhakikisha raia waliomo kwenye maeneo wanayoyadhibiti wanapatiwa hifadhi na ulinzi, kwa kufuatana na kanuni za kiutu za kimataifa, hususan wale raia wahamiaji wa ndani ya nchi 10,000 waliopo karibu na kambi ya vikosi vya ulinzi amani vya UM vya MONUC, katika Rutshuru, [kilomita 80 kutoka mji wa Goma].