UNHCR yaomba milioni $92 kwa wahamiaji wa Usomali katika Kenya
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limetoa mwito wa kutaka lifadhiliwe msaada wa dola milioni 92 ili kufarajia kihali Wasomali 250,000 waliosibika na matatizo ya makazi kwenye kambi kongwe za wahamiaji za Dadaab, ziliopo Kenya mashariki, karibu na mipaka na Usomali.