24 Disemba 2008
Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) mapema wiki hii limetiliana sahihi na Jeshi la Sudan, pamoja na Halmashauri ya Taifa juu ya Ustawi wa Watoto, ile Taarifa ya Mafahamiano yenye kuahidi watoto wote, pote nchini, watapatiwa hifadhi imara na madhubuti katika Sudan.