Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana wanaoishi na VVU Namibia/Tanzania wahitajia mchango wa kitaaluma skulini mwao

Vijana wanaoishi na VVU Namibia/Tanzania wahitajia mchango wa kitaaluma skulini mwao

Matokeo ya utafiti wa karibuni, uliodhaminiwa na UM kuchunguza mahitaji ya wanafunzi vijana na watoto wanaoishi na virusi vya UKIMWI katika mataifa ya Namibia na Tanzania, yameonyesha mara nyingi kundi hili dhaifu kiafya, hunyimwa misaada wanayohitajia kujiendeleza kiilimu.