30 Disemba 2008
Shirika la Afya Duniani (WHO), kwenye taarifa iliochapishwa Ijumanne ya leo, limeonya ya kuwa mamia ya majeruhi katika hospitali za Tarafa ya Ghaza wanakabiliwa na hatari ya ongezeko kubwa la vifo vinavyozuilika, kwa sababu ya ukosefu wa madawa.