WFP itafadhilia posho ya mwezi kwa waathiriwa wa vurugu Goma
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetangaza kwamba kuanzia Ijumatano ya kesho litaendeleza ugawaji wa posho ya chakula cha siku 10 kwa waathiriwa 135,000 ziada waliopo kwenye kambi sita za wahamiaji wa ndani karibu na mji wa Goma.