KM ameteua mjumbe maalumu kusuluhisha mgogoro wa JKK
KM Ban Ki-moon amemteua raisi mstaafu wa Nigeria, Jenerali Olusegun Obasanjo, kuwa Mjumbe Maalumu atakayeshughulikia juhudi za kutafuta suluhu ya kuridhisha kuhusu mzozo uliofumka wiki za karibuni katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK).