Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raisi wa Baraza la Haki za Binadamu anahimiza subira juu ya kazi zake

Raisi wa Baraza la Haki za Binadamu anahimiza subira juu ya kazi zake

Raisi wa Baraza la UM juu ya Haki za Binadamu, Martin IHOEGHIAN UHOMOIBHI wa Nigeria alipowasilisha ripoti yake Ijumanne mbele ya Baraza Kuu juu ya kazi ya taasisi anayoiongoza, alitahadharisha wajumbe wa kimataifa wawe na subira kabla ya kutoa maamuzi juu ya namna shughuli za Baraza zinavyotekelezwa, kwa sababu bodi hilo linashuhudia siku za mwanzo za hatua za mabadiliko katika shughuli zake.