Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP inapendekeza ifadhiliwe tani 55,000 za chakula, kuhudumia waathiriwa wa mapigano

WFP inapendekeza ifadhiliwe tani 55,000 za chakula, kuhudumia waathiriwa wa mapigano

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) linakadiria jumla ya watu waliong’olewa makazi katika eneo la mashariki, katika JKK, inapindukia milioni 1.3 (moja na laki tatu); na tani za chakula zinazohitajika kuwakidhia watu hawo mahitaji yao kuanzia kipindi cha sasa hadi mwishoni Aprili 2009 ni tani 55,000, ambao utaigharimu jumuiya ya kimataifa dola milioni 61. ~~