Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa Nairobi juu ya JKK waamrisha mapigano yasitishwe, halan

Mkutano wa Nairobi juu ya JKK waamrisha mapigano yasitishwe, halan

Mwisho wa wiki iliopita wajumbe waliohudhuria mkutano wa Nairobi ulioandaliwa na Umoja wa Afrika kuzingatia mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mkutano ambao uliungwa mkono na UM na kuhudhuriwa na KM Ban Ki-moon, walitoa taarifa maalumu ya pamoja, ilioyanasihi makundi yanayohasimiana kusimamisha mapigano yao haraka katika eneo la mashariki na kuyataka yashirikiane kwenye majadiliano ya kusluhisha mvutano wao kwa njia ya amani.