WHO imeonya juu ya hasara ya kuinyima sekta ya afya misaada ya maendeleo
Dktr Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametoa taarifa maalumu yenye kuhadharisha serikali za kimataifa na viongozi wa kisiasa kutopwelewa kwenye zile juhudi zao za kuhudumia bora sekta za afya, hasa katika mazingira ya soko la kimataifa liliovamiwa na mgogoro wa fedha na uchumi.