Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Matumizi ya dini kuhalalisha ugaidi, na mauaji ya wasiodhuru, yapingwa kidhati na kikao maalumu cha BK

Matumizi ya dini kuhalalisha ugaidi, na mauaji ya wasiodhuru, yapingwa kidhati na kikao maalumu cha BK

Mkutano wa siku mbili wa Baraza Kuu, uliohudhuriwa na wawakilishi wote, kuzingatia juhudi za kuimarisha “Utamaduni wa Amani” ili kukomesha hali duni na mitafaruku duniani na kukuza maelewano na mafahamiano miongoni mwa nchi wanachama, kikao hicho kilihitimishwa Alkhamisi usiku ambapo wajumbe wa kimataifa waliafikiana kupinga matumizi ya dini kuhalalisha vitendo vya mauaji ya watu wasio hatia, na pia kulaani vitendo vya kigaidi.