18 Novemba 2008
Ofisi ya UM Inayohusika na Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti watu 25,000 waliong’olewa makazi wamekusanyika kwenye kambi ya walinzi amani wa MONUC, ya Bambu, iliopo kilomita 80 kaskazini ya mji wa Goma kutafuta hifadhi na misaada ya kihali, kwa sababu kwenye jimbo lao kumekosekana mashirika ya kimataifa yanayohudumia misaada ya kiutu kwa waathiriwa wa vurugu liliopamba majuzi kwenye eneo lao.~~