Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtaalamu Huru wa UM juu ya Haki za Binadamu ahadharisha mateso yamepamba vizuizini Guinea-Bissau

Mtaalamu Huru wa UM juu ya Haki za Binadamu ahadharisha mateso yamepamba vizuizini Guinea-Bissau

Manfred Nowak, Mkariri Maalumu wa UM juu ya Mateso na adhabu nyengine katili zinazodhalilisha utu, baada ya kumaliza ziara yake katika taifa la Guinea-Bissau, aliwaambia waandishi habari ya kwamba raia wanaojikuta kwenye vizuizi vya polisi katika taifa hilo [mara nyingi] huteswa na kusumbuliwa kwa mpangalio, na wakati huo huo wafungwa huadhibiwa kikatili kabisa, hali ambayo anaamini inasababishwa na kuharibika kabisa kwa mfumo wa sheria katika nchi. Alisema wafungwa wa kisiasa, pamoja na wale watuhumiwa wa uhalifu wa kawaida, wote huteswa na polisi katika Guinea-Bisaau, [pale wanaposhikwa na hulazimishwa] wakubali kukiri makosa bila ushahidi wala kupelekwa mahakamani.~~