UM umetangaza ombi la kutaka ufadhiliwe dola bilioni 7 kuhudumia kidharura watu milioni 30 katika 2009
Ijumatano KM Ban Ki-moon amewasilisha mjini Geneva, waraka maalumu wenye ombi linalotaka jamii ya kimataifa ifadhilia UM msaada wa dola bilioni 7 ili kushughulikia huduma za dharura, za kiutu, katika 2009, kwa watu milioni 30 wanaoishi katika nchi 31 duniani.