Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICC imetoa warka wa kushikwa makamanda watatu waasi Darfur

ICC imetoa warka wa kushikwa makamanda watatu waasi Darfur

Luis Moreno Ocampo, Mwendesha Mashitaka wa Mahkama ya UM Juu ya Jinai ya Halaiki (ICC) ametoa hati ya kuwashika makamanda watatu wa vikosi vya waasi wa Darfur, kwa kuhusika na mashambulio yaliofanyika mwezi Septemba mwaka jana katika eneo la Haskanita ambapo walinzi amani 12 wa Umoja wa Afrika waliuawa na 7 walijeruhiwa, na wakati huo huo magari 17 ya UA yalitekwa nyara kambini kwao.