Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kuhamasisha Maendeleo ya Viwandani Afrika

Siku ya Kuhamasisha Maendeleo ya Viwandani Afrika

UM unaadhimisha Siku ya Kukuza Maendeleo ya Viwanda Afrika. Risala ya KM kuihishimu siku hii ilitilia mkazo ya kuwa shughuli za kukuza viwanda katika Afrika ikitekelezwa itaashiria hatua itakayosaidia pakubwa kudhibiti, kwa mafanikio, matatizo ya chakula, fedha na athari za mabadiliko ya hali ya hewa na, hatimaye, kuimarisha maendeleo ya kiuchumi na jamii ili kuufyeka umaskini katika bara hilo.