Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkataba wa kupiga marufuku mabomu yaliotegwa ardhini unafanyiwa mapitio Geneva

Mkataba wa kupiga marufuku mabomu yaliotegwa ardhini unafanyiwa mapitio Geneva

Mjini Geneva, Uswiss kulifunguliwa rasmi, leo hii, kikao cha 9 cha Mataifa Yalioidhinisha Mkataba wa Kupiga Marufuku Mabomu Yaliotegwa Ardhini ambapo risala ya Raisi wa mkutano, Balozi Jurg Streuli ilikumbusha kwamba licha ya kuwa mabomu milioni 40 ya kutega yalifanikiwa kuangamizwa kimataifa, mapaka sasa, na wakati huo huo kilomita kadhaa za ardhi zilifufuliwa baada ya mabomu hayo kuteketezwa, hata hivyo majukumu makubwa na mazito bado yamesalia na yatakikana kufyeka silaha hizi ovu katika maeneo kadha wa kadha ya dunia.