Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Twamkumbuka Mama Afrika - Miriam Makeba

Twamkumbuka Mama Afrika - Miriam Makeba

Tarehe 27 Novemba 2008 ni Siku Kuu ya Kutoa Shukrani nchini Marekani, na kawaida ofisi zote hufungwa, ikijumuisha vile vile ofisi za Makao Makuu ya UM, ziliopo jiji la New York, Marekani. Hata hivyo, Idhaa ya Kiswahili ya Redio ya UM imewajibika kutayarisha vipindi katika siku hii. Ilivyokuwa hii ni Siku Kuu ya Kutoa Shukrani, nasi pia tumeamua kuandaa makala maalumu, yenye kuwasilisha shukrani za jumuiya ya kimataifa, kwa ujumla, kuhusu mchango wa Balozi Mfadhili wa Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO), Mama wa Afrika, msanii maarufu wa Afrika Kusini, marehemu Miriam Makeba katika kuhudumia kihali umma uliokabiliwa na matatizo ya ufukara na hali duni.~

Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.