Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ripoti ya UM inasema ukamataji wa kihorera Sudan umetanda nchi nzima

Ripoti ya UM inasema ukamataji wa kihorera Sudan umetanda nchi nzima

Ripoti ya Ofisi ya Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu (OHCHR) kuhusu Sudan, iliowasilishwa rasmi leo Ijumaa mjini Geneva, inasema ukamataji wa kihorera wa raia na uwekaji kizuizini kwa watu wasio hatia, umezagaa katika sehemu nyingi za nchi, na ni vitendo ambavyo ripoti ilisema hufungamana na ukiukaji wa haki za binadamu unaoambatana na watu kuteswa na vitendo vyengine vya uoenevu na unyanyasaji.