Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kimataifa kuhishimu watu wa umri mkubwa

Siku ya Kimataifa kuhishimu watu wa umri mkubwa

Tarehe 01 Oktoba huadhimishwa na UM kama ni Siku Kuu ya Watu Wenye Umri Mkubwa. Siku hii hutumiwa na jamii ya kimataifa kukumbushana umuhimu na ulazima wa kuupatia umma wa watu wakongwe hali njema ya afya, raha, ustawi na hishima, mambo ambayo yameonekana kukosekana katika miaka ya karibuni, licha ya kuwa Mataifa Wanachama yalishaahidi kuondosha ubaguzi dhidi ya fungu hili kubwa, na muhimu, katika jamii zao, umma ambao kila siku hunyimwa haki halali za kimsingi.~~