Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kamati ya Nne imeafikiana kusailia amani, ukoloni na masuala maalumu ya kisiasa

Kamati ya Nne imeafikiana kusailia amani, ukoloni na masuala maalumu ya kisiasa

Kamati ya Nne ya Baraza Kuu inayozingatia Masuala Maalumu ya Kisiasa na Kuondosha Ukoloni ilikutana kwenye mkutano mfupi Alkhamisi, na ilipitisha ajenda ya kusailiwa kwenye kikao cha mwaka huu, ambapo zaidi ya mada 12 zitajadiliwa, zikijumuisha vie vile masuala juu ya matumizi ya amani ya sayari nyengine, nje ya dunia, operesheni za ulinzi amani za UM na uondoshaji wa ukoloni kwenye Maeneo Yasiojitawala. ~