Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Makazi Bora 2008

Siku ya Makazi Bora 2008

Shirika la UM juu ya Makazi (UN-HABITAT) kila mwaka huiadhimisha Ijumatatu ya mwanzo wa mwezi Oktoba kuwa ni Siku ya Makazi Bora Duniani. Lengo la taadhima hizi ni kutathminia hali ya miji na haki za kimsingi za mwanadamu kupatiwa makazi ya kiutu kwa wote, pamoja na jukumu la jamii ya kimataifa katika kuyatekeleza hayo.