Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNHCR atetea haki za mafakiri na wahamaji waliokosa makazi ulimwenguni

Mkuu wa UNHCR atetea haki za mafakiri na wahamaji waliokosa makazi ulimwenguni

António Guterres Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Wahamiaji (UNHCR) kwenye risala ya ufunguzi mbele ya wajumbe waliohudhuria mkutano wa mwaka Geneva wa Kamati ya Utendaji ya UNHCR, ya kwamba maslahi ya watu mafukara na wale waliong’olewa makwao ulimwenguni yamo hatarini sasa hivi, kwa sababu ya mchanganyiko wa athari mbalimbali zinazochochewa na migogoro iliofumka karibuni ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, hali ambayo, alisema anakhofia itazusha watu kungo’lewa zaidi makazi katika miaka ijayo.