Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM wakumbusha 'walio vizuizini wana haki za kiutu na lazima zihishimiwe'

UM wakumbusha 'walio vizuizini wana haki za kiutu na lazima zihishimiwe'

Kamisheni ya UM juu ya Haki za Binadamu imeanzisha kampeni maalumu ya kimataifa itakayoendelezwa hadi Oktoba 12 (2008) ambapo taasisi za kizalendo zinazogombania haki za binadamu katika nchi wanachama wa UM, pamoja na mashirika yasio ya kiserikali na wadau wengine husika zitajumuika kukumbushana juu ya ulazima, na umuhimu, wa kuhakikisha watu waliowekwa vizuizini na kwenye magereza huwa wanatekelezewa haki zao zote halali za kimsingi.