Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mafukara wa kimataifa wahakikishiwa misaada hakika na KM wa UM kumudu maisha

Mafukara wa kimataifa wahakikishiwa misaada hakika na KM wa UM kumudu maisha

Wakati nikielekea studio KM Ban Ki-moon alikuwa na mkutano wa kila mwezi na waandishi habari wa kimataifa. Kwenye risala yake ya ufunguzi alisema mafukara na maalhakiri wa kimataifa wana haki ya kutegemea UM na Mataifa Wanachama kuwasaidia kustawisha maisha yao, licha ya kuwa ulimwengu sasa hivi umekabiliwa na matatizo ya fedha katika soko la kimataifa.