Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu ahimiza hifadhi bora kwa wageni Afrika Kusini baada ya mauaji katili

Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu ahimiza hifadhi bora kwa wageni Afrika Kusini baada ya mauaji katili

Navanethem Pillay, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu (OHCHR), amelaani vikali mauaji ya kikatili yaliotukia Ijumaaa iliopita katika kijiji cha Eastern Cape, Afrika Kusini ambapo Sahra Omar Farah, mama wa KiSomali pamoja na watoto wake wawili wa kiume wajane, ambao mmoja wao alikuwa kiziwi, na vile vile binti wake wa miaka 12 waliuawa kikatili kwa visu na marungu karibu na duka liliokuwa linaendeshwa na Msomali.