Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ofisa wa UNHCR anasema hifadhi ya wahamiaji duniani inaregarega

Ofisa wa UNHCR anasema hifadhi ya wahamiaji duniani inaregarega

Erika Feller, Kamishna Mkuu Mdogo wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) aliwaambia wawakilishi kutoka mataifa 76 wa Kamati ya Utendaji ya Shirika ambayo inakutana Geneva kwa sasa, ya kwamba licha ya kupatikana mafanikio mwaka uliopita kuhusu utekelezaji wa haki za kibinadamu na kiutu za kuwapatia wahamiaji ulimwenguni hifadhi inayofaa, hata hivyo imethibitika kihakika vile vile ya kwamba idadi kubwa ya wahamiaji pamoja na wale watu wenye kuomba hifadhi ya kisiasa, katika sehemu mbalimbali za dunia bado wanaendelea kukabiliwa na utovu wa ustahamilivu dhidi yao na hunyimwa haki zao halali, pia, hali ambayo inakwenda kinyume kabisa na kanuni rasmi za kimataifa juu ya wahamiaji ambazo zinawahakikishia haki hizo. ~~