Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waziri wa zamani Rwanda ahamishiwa kizuizini Arusha

Waziri wa zamani Rwanda ahamishiwa kizuizini Arusha

Waziri wa zamani wa Miradi ya Nchi Rwanda, Augustin Ngirabatware, anayekabili mashitaka ya kushiriki kwenye mauaji ya halaiki na ukiukaji mbaya wa kanuni za kiutu za kimataifa, Ijumatano amehamishwa kutoka Frankfurt, Ujerumani, alipokamatwa wiki mbili zilizopita, na kupelekwa kwenye Kituo cha Kufungia Watu cha Mahakama ya Kimataifa juu ya Rwanda (ICTR) kilichopo Arusha, katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.