Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakulima wa kiasilia warahisishiwa biashara na UM

Wakulima wa kiasilia warahisishiwa biashara na UM

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limetangaza vyombo viwili vipya vya kuwasaidia wakulima wanaotumia mbolea za kimaumbile kuuza bidhaa zao kwenye soko la kimataifa bila ya pingamizi. Vifaa hivi ni matunda ya ushirikiano wa utafiti wa miaka sita miongoni mwa wataalamu wa FAO, Shirika la UM juu ya Maendeleo na Biashara (UNCTAD) na pia Shirikisho la Kimataifa la Wakulima Wanaotumia Mbolea za Kimaumbile (IFOAM) na vinatarajiwa kuwasilisha mapokezi bora ya mazao yaliyooteshwa kimaumbile katika soko la kimataifa.