Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ngirabatware amekana makosa ya jinai ya halaiki Rwanda

Ngirabatware amekana makosa ya jinai ya halaiki Rwanda

Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) imeripoti ya kwamba Augustin Ngirabatware, aliyekuwa Waziri wa Mipango ya Nchi Rwanda Ijumaa alipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza kukabili mashitaka alikana makosa kumi ya kushiriki kwenye mauaji ya halaiki nchini mwao katika miaka ya 1990, jinai ambayo inasemekana ilikiuka sheria ya kiutu ya kimataifa.