Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR ina wahka juu ya usalama wa wahamiaji wa ndani katika JKK

UNHCR ina wahka juu ya usalama wa wahamiaji wa ndani katika JKK

UM umeripoti kuwa na wasiwasi mkuu juu ya usalama wa umma uliopo kwenye eneo la vurugu karibu na Goma, katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK). Ron Redmond Msemaji wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) aliwaambia waandishi habari Geneva Ijumaa kwamba wamepokea habari za kushtusha kuhusu hali ya wahamiaji wa ndani waliopo Rutshuru, mji wa Kivu Kaskazini uliopo kilomita 90 kutoka Goma.~~