Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNEP imenasihi ajali zisokwisha za kimaumbile zaweza kukomeshwa panapo udhibiti bora wa hali ya hewa

UNEP imenasihi ajali zisokwisha za kimaumbile zaweza kukomeshwa panapo udhibiti bora wa hali ya hewa

Achim Steiner, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) leo ametoa taarifa iliohadharisha kwamba pindi mabadiliko ya hali ya hewa yatashindwa kudhibitiwa kama inavyostahiki kisayansi, kuna hatari ya maaafa ya kimaumbile kukithiri na kuathiri kihali na mali umma wa kimataifa, kama ilivyotukia wiki hii katika mji wa New Orleans, Marekani ambapo Kimbunga Gustav kilisababisha maelfu ya watu kuhamishwa makwao na kupelekwa kwenye maeneo salama.