Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa DPI/NGO Paris unazingatia biashara haramu ya watoto

Mkutano wa DPI/NGO Paris unazingatia biashara haramu ya watoto

Mkutano wa Idara ya Habari ya UM na mashirika yasio ya kiserikali unaofanyika Paris, Ufaransa katika siku ya pili ya majadiliano, Alkhamisi mashauriano yalilenga zaidi kwenye tatizo la biashara karaha ya watoto wadogo ambao hutekwa nyara na majambazi,na baadye huvushwa mipaka kutopka makwao na hutumiwa kwenye vitendo haramu vyenye kuwanyima watoto hao haki za kimsingi na utu wao. Mathalan, watoto hawa wenye umri mdogo hulazimishwa kufanya kazi zisiolingana na umri wao, na mar nyengine hushirikishwa kwenye vitendo karaha vya kuwafanya watoto hawa kuwa watumwa wa uzinzi. ~