Uharamia Usomali wamtia kiherehere Mjumbe wa KM
Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali, Ahmmedou Ould Abdallah amesema ameshtushwa sana kwa kuongezeka kwa uharamia kwenye mwambao wa Usomali, kitendo ambacho alisisitiza kinahatarisha utulivu kurejea kwenye eneo hilo la Pembe ya Afrika.