Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF imeonya, watoto milioni 3 wa Pembe ya Afrika wanakabiliwa na utapiamlo hatari

UNICEF imeonya, watoto milioni 3 wa Pembe ya Afrika wanakabiliwa na utapiamlo hatari

Per Engebak, Mkurugenzi wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) kwa ukanda wa Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki amenakiliwa akisema watoto karibu milioni 3 wanaoishi kwenye maeneo ya Pembe ya Afrika wanakabiliwa na hatari maututi ya utapiamlo mbaya na maradhi kadha wa kadha, kwa sababu ya kupungua kwa misaada inayofadhiliwa eneo hilo kutoka wahisani wa kimataifa.