Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hapa na Pale

Hapa na Pale

Naibu KM Asha-Rose Migiro alipohutubia mjadala kuhusu tatizo la UKIMWI katika eneo la Afrika kusini ya Sahara alikumbusha kwamba janga hili ovu la UKIMWI “linamomonyoa” ustawi wa maendeleo yaliofikiwa baada ya uhuru, katika sehemu nyingi barani humo. Mkutano uliandaliwa bia na Chuo Kikuu cha UM pamoja na Chuo Kikuu cha Cornell, katika Jimbo la New York na ulifanyika kwenye ukumbi wa Dag Hammarskjöld wa Makao Makuu ya UM. Aliwahimiza wataalamu juu ya VVU/UKIMWI kulenga juhudi zao kwenye taaluma manufaa itakayowasilisha uamuzi wa vitendo utakaochangisha moja kwa moja kwenye vita dhidi ya maradhi maututi ya UKIMWI.