Coomaraswamy anasihi hifadhi bora kwa watoto walionaswa kwenye mazingira ya uhasama
Mjumbe Maalumu wa KM juu ya Hifadhi ya Mtoto katika Mazingira ya Vita na Mapigano, Radhika Coomaraswamy Ijumanne alihutubia Baraza la Haki za Binadamu linalokutana mjini Geneva, ambapo alikumbusha watoto karibu 300,000 walilazimishwa kujiunga, kama wapiganaji, na makundi kadha ya wanamgambo yanayoshiriki kwenye vurugu na uhasama katika sehemu kadha wa kadha za dunia.