Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Matumizi ya madawa ya usanisi yameshuhudiwa kuongezeka katika nchi zinazoendelea, UNODC yaripoti

Matumizi ya madawa ya usanisi yameshuhudiwa kuongezeka katika nchi zinazoendelea, UNODC yaripoti

Ofisi ya UM juu ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya na Uhalifu (UNODC) imebainisha kwenye ripoti ya \'Tathmini ya 2008 juu ya Madawa ya Kulevya Yanayotumiwa kama Viburudisho Duniani\' kwamba matumizi ya yale madawa ya usanisi ya anasa – kama "amphetamine, metamphetamine (meth) na ecstasy" – yamebainika kuzidi katika nchi zinazoendelea, hasa katika maeneo ya Mashariki na Kusini-Mashariki ya Bara la Asia na katika Mashariki ya Kati.