Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UM anayesimamia misaada ya dharura anasihi fujo isistishwe Darfur

Mkuu wa UM anayesimamia misaada ya dharura anasihi fujo isistishwe Darfur

John Holmes, Naibu KM juu ya Masuala ya Kiutu na Mshauri wa KM kuhusu Misaada ya Dharura amenakiliwa akisema ana wasiwasi mkubwa juu ya ripoti alizopokea kuhusu kuendelea kwa fujo na vurugu katika Darfur. Alisema ripoti zimeonyesha karibuni kulifanyika mashambulio ya kijeshi katika Darfur Kaskazini na Jebel Marra, ikijumuisha mashambulio ya anga katika maeneo ya Birmaza na Disa na pia hujumu kadha dhidi ya wahudumia misaada ya kiutu zinazoendelezwa na makundi yenye kuchukua silaha.