Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IAEA inaashiria kuongezeka kwa matumizi ya umeme unaozalishwa na nyuklia katika miaka ijayo

IAEA inaashiria kuongezeka kwa matumizi ya umeme unaozalishwa na nyuklia katika miaka ijayo

Ripoti iliochapishwa rasmi na Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA), na kutangazwa Alkhamisi (11/09/08) ilibashiria ya kwamba matumizi ya nishati ya nyuklia duniani yataongezeka kwa mara mbili zaidi katika miongo miwili ijayo, kushinda kima cha hivi sasa, kwa sababu ya kukithiri kwa mahitaji ya nishati ulimwenguni.