11 Septemba 2008
Ripoti iliochapishwa rasmi na Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA), na kutangazwa Alkhamisi (11/09/08) ilibashiria ya kwamba matumizi ya nishati ya nyuklia duniani yataongezeka kwa mara mbili zaidi katika miongo miwili ijayo, kushinda kima cha hivi sasa, kwa sababu ya kukithiri kwa mahitaji ya nishati ulimwenguni.