Waathiriwa walionajisiwa kimabavu JKK wavunja ukimya wa mateso yao hadharani
Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) likijumuika na kundi la wanaharakati wa Marekani wanaogombania haki za wanawake, wa kutoka Jumuiya ijulikanayo kama V-Day, wametayarisha warsha mbili muhimu katika miji ya Goma na Bukavu, ikiwa miongoni mwa kampeni za pamoja kukabiliana na matatizo ya udhalilishaji wa kijinsia katika JKK ambapo, mara nyingi wanawake hukamatwa kimabavu na kunajisiwa.