Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raisi mpya wa BK ahimiza demokrasia ihuishwe katika UM

Raisi mpya wa BK ahimiza demokrasia ihuishwe katika UM

Raisi mpya wa Baraza Kuu la UM, Miguel D’Escoto Brockmann, aliyekuwa Waziri wa Nchi za Nje wa Nicaragua, jana jioni alifungua rasmi kwenye Makao Makuu ya UM kikao cha 63 kinachojumuisha Mataifa Wanachama 192 kutoka kila pembe ya dunia, ambapo wajumbe wao hukusanyika kila mwaka, kuanzia mwezi Septemba hadi Disemba, kuzingatia masuala yote muhimu ya kimataifa, na kuchukua maamuzi kwa kulingana na kanuni za Mkataba wa UM.

Sikiliza kwenye idhaa ya mtandao taarifa zaidi.