Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNIFEM inasema serikali na mashirika ya kimataifa yanawajibika kukamilisha ahadi za MDGs

UNIFEM inasema serikali na mashirika ya kimataifa yanawajibika kukamilisha ahadi za MDGs

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Wanawake (UNIFEM) kwenye ripoti iliowakilishwa rasmi kwenye Makao Makuu ya UM Alkhamisi ya leo, ilieleza kwamba usawa wa kijinsia hauwezi kukamilishwa kama ilivyopendekezwa na Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) bila ya kuwepo uwajibikaji wa nguvu utakaosaidia kukamilisha ahadi zilizotolewa kusukuma mbele maendeleo ya wanawake.