Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama linazingatia Chad na JAK

Baraza la Usalama linazingatia Chad na JAK

Amani na Usalama

Baraza la Usalama Ijumaa limezingatia ripoti ya karibuni ya KM juu ya hali ya usalama katika Chad na Jamhuri ya Afrika ya Kati (JAK). Ndani ya ripoti KM amependekeza UM upeleke vikosi vya kulinda amani vya UM vya wanajeshi 6,000 wanaotakikana kuchukua nafasi ya vikosi vya Umoja wa Ulaya viliopo Chad mashariki na kaskazini-mashariki ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, maeneo ambayo katika miaka ya karibuni yaliharibiwa na fujo na vuruguu, na kusababisha halaiki ya raia kungo’lewa makazi na kuelekea kwenye maeneo mengine walipopatiwa uhamisho wa muda.~