Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Katibu Mkuu apongeza mafanikio ya kikao maalumu cha MDGS

Katibu Mkuu apongeza mafanikio ya kikao maalumu cha MDGS

Baada ya mikutano ya ngazi za juu pamoja na warsha kadha wa kadha zilizofanyika siku nzima hapa Makao Makuu, Alkhamisi ya jana, kupitia namna utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) unavyoendelezwa, wajumbe waliowakilisha serikali, taasisi za kimataifa, jumuiya za kiraia na mashirika ya wafanyabiashara waliungana kipamoja na kuitika mwito wa kuchukua hatua za utendaji wa dhahrura ili kupunguza, kwa kima kikubwa, itakapofika 2015, janga la ufukara, njaa iliokithiri, magonjwa yanayozuilika na maafa mengine ya kiuchumi na jamii yenye kusumbua umma wa nchi zinzoendelea.