Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raia wa Usomali 52 wakadiriwa kufariki kwenye Ghuba ya Aden, UNHCR

Raia wa Usomali 52 wakadiriwa kufariki kwenye Ghuba ya Aden, UNHCR

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti wanakadiria raia wa Usomali 52 walifariki, [wiki iliopita] baada ya mashua iliotumiwa kuwavusha kimagendo kuelekea Yemen ilipoharibika na kuyoyoma kwa siku 18 bila ya chakula wala maji kwenye Ghuba ya Aden.