Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waziri wa Nchi za Kigeni wa Urusi kuliambia BK 'usalama wa Abkhazia na Ossetia Kusini sasa utadhaminiwa kihakika'

Waziri wa Nchi za Kigeni wa Urusi kuliambia BK 'usalama wa Abkhazia na Ossetia Kusini sasa utadhaminiwa kihakika'

Majadiliano ya jumla kwenye kikao cha Baraza Kuu cha wawakilishi wote bado yanaendelea Makao Makuu na yameingia siku ya sita.~~ Lakini kwenye mjadala wa siku ya tano, Ijumamosi, Waziri wa Nchi za Kigeni wa Shirikisho la Urusi, Sergey V. Lavrov alwaambia wawakilishi wa kimataifa usalama wa majimbo yaliojitenga katika Georgia, ya Abkhazia na Ossetia Kusini, sasa utadhaminiwa kihakika baada ya taifa lake kutambua uhuru wa maeneo hayo. ~