Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naibu mkurugenzi wa IAEA anazuru Iran

Naibu mkurugenzi wa IAEA anazuru Iran

Naibu Mkurugenzi wa Shirika la IAEA, Olli HEINONEN, ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Usalama amewasili Teheran Alkhamisi, kwa ziara maalumu ya siku mbili. Anatarajiwa kuongoza mazungumzo na maofisa wa vyeo vya juu wa Iran wanaohusika na sera za matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia.~