KM atoa ujumbe maalumu wa amani kuhishimu olimpiki
KM Ban Ki-moon ametoa taarifa maalumu leo inayoambatana na kufunguliwa rasmi kwa michezo ya olimpiki mjini Beijing, Uchina inayorudia tena nasaha za kabla,zilizopendekeza kuwepo maafikiano, miongoni mwa makundi yote yanayohasimiana, kusitisha vita, uhasama na mapigano wakati mashindano ya riadha yanaendelezwa mnamo wiki mbili zijazo.